Wednesday, February 16, 2011

Jane Mihanji (kulia) na mimi tukipiga story wakati wa Bonanza la Waandishi wa Habari lililoandaliwa na Kampuni ya Airtel liliofanyika katika viwanja vya Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Mdau Balegeya akitafakari mambo yalivykuwa yakijiri katika viwanja hivyo kama anavyoonekana akiwa katika pozi kali la picha.

Wadau Dada Winn na kaka Mohamed, wakishangaa jambo katika viwanja hivyo, walikuwa wakipiga story hamad wakastukio jambo lililowaacha mdomo wazi ambalo lilikuwa likifanywa na mmoja wa wanahabri amabye hayupo pichani.


Kadaaaa Khadija akijaribu kuzirudi ngoma za msondo zilizokuwa zikipigwa viwanjani hapo kama anavyoonekana kulia kwa huyo mdada anaye dansi naye.


Wadau kutoka kushoto Ester Mvungi, Rhodar Kangero na Selina Wilsoni, walikuwa miongoni mwa wanahabari kutoka Uhuru Publictaions Ltd, waliojitosa katika bonanza hilo.


Msondo waliwakuna wengi, mmoja wapo ni brother Mohamed kama anavyoonekana akilisakata rhumba la Msondo.



Katika bonanza hilo, kulishindaniwa michezo mbalimbali, UPL hawakubaki nyuma, walijitosa katika mchezo wa kuvuta kamba ambapo walifanikiwa kulitwaa kombe kama wanavyoonekana wakijidai na kombe hilo!!!!!!!





No comments: