Tuesday, July 31, 2012


Sijaridhishwa na matokeo
Tusker Project Fame -Msechu


Fahamu jumapili iliyopita July 29 2012 ndio shindano la Tusker Project fame 2012 limemalizika, washindi waliotangazwa ni Mkenya Ruth alieshika nafasi ya kwanza, wa pili pia ni Mkenya Doreen na watatu ni Mrwanda Jackson.

Matokeo ni maamuzi ya majaji pamoja na kura lakini mshindi wa Tusker All stars kutoka Tanzania, Peter Msechu ameeleza ni sehemu gani ya matokeo hayo ambayo hajakubaliana nayo.

Ameamplfy “Ruth kama mshindi alistahili kushinda kwa sababu hata rekodi yake toka ameanza ilikua nzuri, tukija katika kuimba Doreen alieshika nafasi ya pili sidhani kama ilimfaa na niseme Jackson alionyesha uwezo wake siku zikiwa zimeisha ila kama ni ishu ya kuperform na kuimba Doreen hakutakiwa kuwa namba 2, ilitakiwa akae nafasi ya tatu kwa sababu hana uwezo kama Jackson, Jackson nampa namba 2 alafu Doreen ndio tatu”

No comments: