Monday, August 20, 2012

Diwani afuturisha wafanyakazi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd
DIWANI wa Kata ya Kwadelo,wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma, Omary Kariati (wa pili kushoto), akitoa neno wakati wa futari aliyowaandalia wafanyakazi wa Kampuni ya Uhuru Pulbications Limited (UPL), wachapishaji wa magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, ofisi za UPL, Lumumba, Dar es Salaam, Mwishoni mwa wiki iliyopita.


Mapishi ya Biriani ya kuku iliyopambwa kwa mayai

Birini ni moja ya chakula ambacho watu wengi hupenda kukitumia nyakati za sikukuu kama chakula maalumu.
Wengi katika siku kama hizi, hawapendi kukisa kabisa.
Hata hivyo, upishi wa chakula hutofautiana. Mimi leo nawapikia biriani ya nyama ya kuku ambayo nitaipamba kwa mayai.


MAHITAJI;
Mchele kilo moja aina ya Pishori/Basmati
Kuku aliyechinjwa mmoja, mkate vipande vya kawaida
Paketi moja ya maziwa ya mtindi
Vitunguu maji vikubwa sita, vikate vipande vikubwa vya mviringo
Mayai sita
Vitunguu swaumu vilivyopondwa kijiko kimoja cha chai.
Tangawizi mbichi iliyotwangwa kijiko kimoja cha chai.
Malimao makubwa mawili
Papai bichi moja, limenye, toa mbegu, kata vipande na kisha lisage kwenye blenda kwa kutumia jagi linalotoa chembe kubwa kubwa.
Viazi mviringo vikubwa kama 5, vimenye uvikate nusu.
Nyanya ziloiva, zisage pia kisha uzichuje
Tomato paste kiasi, mafuta ya kupikia, kiasi, Chumvi kiasi, Cinnamon, Pilipili manga kiasi, Karafuu kiasi, Hiliki kiasi na Zafarani kiasi, iloweke katika maji ya moto nusu glass.

NAMNA YA KUPIKA;

Weka ndani ya blender Tangawizi, papai ilosagwa na kitunguu swaumu na maziwa mgando, uvisage mpaka viwe mchanganyiko mzito, Weka pembeni
Osha nyama ya kuku kisha ipake chumvi ukamulie malimao, mwagia mchanganyiko wa papai na tangawizi na vitunguu swaumu kisha weka jikoni uchemshe mpaka iive iwe laini (kama ni kuku ya kienyeji), ikiwa ni kuku wa kizungu usiichemshe sana itavurugika.
Kisha saga tena viungo vyote vilivyosalia pamoja, na umiminie kwenye nyama ya kuku ikiwa inachemka.
Weka nyanya iliyosagwa kwenye blender na ile ya paste kwenye kuku inayochemka, ukoroge ichanganyike kwenye nyama.
Menya vitunguu maji uvioshe uvikate. Weka sufuria jikoni uweke mafuta yachemke.
Kisha tia vitunguu maji ukaange mpaka vibadili rangi na kuwa ya udhurungi, baada ya hapo viipue na uvichuje mafuta uviweke pembeni vipoe.
Menya viazi mviringo uvikaange kwenye mafuta mpaka viive, ipua weka pembeni vipoe
Kama kuku imeiva, isikauke iwe na rojo, chukua vitunguu ulivyokaanga uvimiminue kwenye kuku, na viazi pia, changanya, acha ichemke kiasi halafu ipua weka pembeni tayati kwa kuliwa.
Bandika tena sufuria jikoni utie maji na chumvi, yakichemka tia mchele na mafuta.
Pika kama wali wa kawaida unavyopikwa. Ukishaiva nyunyizia yale maji ya zafarani huku unageuza ili rangi isamba.
Kama huna zafarani basi tumia rangi ya chakula ya orange. Funikia na uweke moto mdogo sana mpaka wali ukauke vizuri (hii ni kama haupalii na mkaa kwa juu.


NB: Kama utapenda unaweza kuweka zabibu kavu pia wakati unaweka mchele kwenye maji ya moto zinaivia humo.

Chemsha pia mayai yakishaiva, yamenye na uyagawanye katikati, yaani vipande viwili, bila kuvuruga kiini cha ndani.
Wali ukiiva, sasa waweza pakua kwenye sinia kubwa na juu ukapanga vipande vya mayai, ili kuleta muonekano mzuri mezani.
Chakula chako mpaka hapo kitakuwa tayari kwa kuliwa.


Karibu sana mezani, na ninawatakia sikukuu njema ya Eid El Fitri.


No comments: